Ruka hadi kwenye maudhui makuu


VISA NA MAFUNZO,
Nilipoanza safari ya kukuandikia wewe msomaji,nilivuta picha ya jambo ninaloenda kulileta kwako.Ama kweli kuna vitu visivyozuilika,na uchungu  pia, upo katika “list” ya vitu visivyozuilika. “hivi kwanini nadondosha chozi?” nilijisemea na kujiuliza kwa muda,hatimaye “ ngoja nijikaze tu!” nilijipa imani nikiamini kuwa huu sio mwisho wasafari,huenda nami yakanikuta  “kama nilisimuliwa pia nimejionea kwa macho yangu,imetokea kuumia namna hii,je,si zaidi kama ikinitokea mimi la!”nilijisemea na kujiuliza pia.Gafla nilizikumbuka jumbe ambazo zimetikisa katika kichwa,nazo pia zipo ndani ya malengo niliyo nayo juu yako msomaji,nilianza kujipa tumaini kwa mbali nikiamini utaenda kukumbana na yaliyomengi ndani ya kijitabu hiki. “Hivi kwa nini ulimfanyia hivyo? Kipndi  chote hicho haukutambua kuwa  maisha yake umeyashikilia mikononi mwako? Umeridhika kuona anataabika na amepoteza mwelekeo na  dira kabisa ya maisha yake!” Kuna tofauti  kubwa kwa mtu Yule anayeliona tukio na kushindwa  kulipa nafasi ya kulitafakari kwa kina,na mtu Yule anayeliona tukio na kulitafakari kwa kina.Kabla sijakupeleka  katika ukurasa mwingine wa maandishi,naomba nikupe kisa kimoja ambacho sio yeye tu,ni wengi huwapata.Alikuwapo  mtu mmoja ambaye alitembelewa  na rafiki yake Asubuhi na mapema.Kama ilivyokawaida,alimkaribisha  rafiki yake kwa furaha na shangwe ya hali ya juu.Walishinda nyumbani pamoja huku wakiendelea “kucheas” pamoja.Mara huyo mchana, na hatimaye jioni “karibu tena” mara alimwaga na kumkaribisha  kwa mara nyingine .Akiwa njiani alikutana na jamaa mwingine,walisalimiana na hatimaye waliagana.Kwa kuwa jamaa huyo alikuwa mtani wa rafiki yake aliyetoka kumtembelea  aliona ni njia pekee ya kumtania kwa kiswali ili akishindwa aweze kumzomea.Haraka alifika kwa mtani wake
                        “hongera chalii wangu,leo umekuwa ma mgeni
                                                (alijibu)
Mara aliulizwa kiswali cha utani,                                
“hivi mgeni wako  alikuwa amevaa nguo ya rangi gani? Je,vipi kuhusu viatu vyake?” ndugu msomaji unaweza kuona swali hilo ni la kipumbafu muno,japokuwa lina maana yake.Mtani alijitwalia ushindi.Swali hilo lilileta utata na hatimaye kuzomewa.Huo ndio uhalisia wa maisha kutokana na vitu au mambo tunayo kutana nayo na kuyaona.Pengine angejipa muda wakufikiria mgeni aliyefika pale nyumbani  na kushinda naye kutwa nzima,sina shaka ,swali hilo lingekuwa rahisi muno.Simlaumu kwani hakujipa muda wa kufikiria kwa undani,ujio wa rafiki yake pale nyumbani.Laiti kama angewaza,angefikiri,angechunguza kwa kina,angegundua masuala mengi juu ya rafiki yake.Suala la kushindwa kutambua rangi ya nguo au viatu,lisingeweza kumpata chalii huyo.
            Nikukaribishe katika ukurasa mwingine wa maandishi,kisa hicho hakiko mbali na jambo ninalolileta kwako,ni jambo rahisi na la kawaida sana.Japokuwa linahitaji kufikiria na kutafakari kwa undani zaidi.Suala la kuliona halina mguso au lina mguso liko juu yako wewe msomaji.
            TAFAKARI yako itakupa radha ya utunzi wa kijitabu hiki “Bado naendelea kukuuliza hivi kwa nini ulimfanyia hivyo? Kipindi chote hicho haukutambua kuwa maisha yake umeyashikilia mikononi mwako? Umeridhika kuona anataabika na amepoteza mwelekeo na dira kabisa ya maisha yake!!”
                        Ukurasa  huu wa maandishi umeambatana na ushauri kwako wewe msomaji.Pengine unapenda kujifunza kitu kupitia maandishi haya.Pengine unatamani  kuwa jasiri pale unapotaka kuanza safari ya maisha yako.Pengine unakatishwa tamaa na hatimaye kupelekea kufa na maono yaliyoko katika kichwa chako,sina shaka kuwa ukinisikiliza mimi ,hutoweza kuanguka kwani sina rekodi ya watu walionisikiliza  na kujulikana kuwa  wamepotea kwa kufuata ushauri wangu.Ndugu tumia “KITABU WATU” hiki ni kitabu ambacho kimeutoa msaada mkubwa ndani ya safari yangu .Ni kitabu ambacho kimetoa faraja kubwa na tumaini katika maisha yangu.Ni kitabu pekee kinachopatikana kila kona ya dunia,kila unapokaa,kitabu hiki utakipata,kila unapotembea,kitabu hiki kipo palepale.Halooo! kila kona,kitabu hiki hujifunua zaidi kukufundisha wewe msomaji wangu.Tumia “ KITABU WATU” kitabadilisha msimamo wa maisha yako.Natumia muda mwingi kuwasoma watu ambao wamepiga hatua Fulani kimaisha,wengine ambao wamenitangulia kutimiza  ndoto kama nilizonazo “Ahsanteh sana Erick Shigongo,street university,umekuwa kitabu bora na umebadilisha mitazamo ya maisha yangu.Maisha yako nimeyageuza kuwa ukurasa wa kitabu,kila siku najitahidi kufungua ukurasa mmojammoja,na kuendelea kujifunza mengi na mengi.Tumia  “KITABU WATU” kitabadilisha msimamo wa maisha yako.Unaamini kuwa palipo na vitoto vichanga,katikati yao kuna kiongozi,unaamini  wanyama  wa mbugani katikati yao kuna kiongozi,unaamini katika msululu wa siafu pia kuna kiongozi? Kama ndiyo,utaniambia hapo ulipo hakuna mtu yeyote wa kugeuza kuwa ukurasa wa kitabu,kila siku ukaufunua na kuendelea kuongeza maarifa? Tumia “KITABU WATU” kitabadilisha msimamo wa maisha yako. “Bado naendelea kukuuliza kwa nini ulimfanyia hivyo? Kipindi chote hicho haukutambua kuwa maisha yake umeyashikilia mikononi mwako?umeridhika kuona anataabika na amepoteza mweleleo na  dira kabisa ya maisha yake!”
                “Unyoya haumdondoki ndege pasina sababu,utamu wa kitabu si maandishi la! Kilichomo ndaniyake,tafakari ni zaidi ya takabari.Hana maana mkosa vyote ajisifupo “nalikuwa nao wapataji tulipo tafuta pamoja”.Thabiti ya neno ni shahada si shuhuda pia salama ni tathimini ya imeishaje”  ukweli wa semi hizi mpenzi msomaji bila kukuchosha,utaupata baada ya kusoma visa vyote ambavyo  utakumbana navyo  ndani ya kijitabu hiki.Pengine bado una  shauku ya kutaka kujua ,taratibu tutafika sehemu ile ya kupata ukweli wa semi hizi. “Bado naendelea kukuuliza kwa nini ulimfanyia hivyo?kipindi chote hicho haukutambua kuwa maisha yake umeyashikilia mikononi mwako? Umeridhika kuona anataabika na amepoteza dira na mwelekeo kabisa wa maisha yake!”
                Mpenzi msomaji,nisikuchoshe,tulipate funzo kidogo,baadae nikupeleke katika vile visa ambavyo vimenisukuma kuandika kijitabu hiki.Jana nilifunga safari na kwenda kumtembelea mzee wangu,sio mzee sana ,hajawa mzee wa makamo,nusu mzee nusu kijana japokuwa anaelekea uzeeni.Ni tegemezi si tegemezi maana yake uchumi wake ni wa kati.Nilikaa nae muda mrefu,baadaye alianza kunipa mawaidha alisema “mchana huu ningekuwa mbali sana,sijui ningekuwa wapi,kama si katika michakaliko basi ningekuwa kwenye starehe ila kama unavyoona,nipo nyumbani nimekaa.Sina nguvu tena,ujana ni muda tu.Ningepata nafasi ya kuambiwa kilichoko uzeeni,haloo,ningepambana kupata ili nije nitumie uzeeni,nisingepika mbegu,ningepanda mbegu  na kuimwagilia ili nije nivune uzeeni lakini muda umepita,natamani kuwa kama wewe kijana japokuwa haiwezikani.Kijana tumia ujana wako vizuri maana umejionea kilichoko uzeeni,alimalizia kwa kusema
                        mkumbuke muumba wako siku za ujana wako,
                   Kabla hazijaja siku zilizo mbaya,         
                   Wala haijakaribia miaka utakaposema,
                   Mimi sina furaha katika hiyo,
                   Kabla jua na nuru na mwezi,
                   Na nyota,havijatiwa giza,
                   Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua,
                   Siku ile WALINZI WA NYUMBA watakapo tetema,
                   Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha ,
                   Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba,
                   Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza,
                   Na milango kufungwa katika njia kuu,
                   Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo,
                   Na hao binti za kuimba watakapopunguzwa” Mzee wangu hakunikaribisha na vinywaji ,vyakula kama wengine wafanyavyo ila tunda alilolipandikiza katika kichwa changu,lilinifanya nipendezwe na ugeni wangu.Jana hiyohiyo sikwenda ukumbi wa starehe nilishinda nyumbani sebuleni nikiwaza yaliyomengi. “Bado naendelea kukuuliza hivi kwa nini ulimfanyia hivyo? Kipindi chote hicho haukutambua kuwa maisha yake umeyashikilia mikononi mwako? Umeridhika kuuna anataabika na amepoteza mwelekeo na dira kabisa ya maisha yake!!”
        Nilimsikia mwingine akisema “sitaki nipate ‘certificate’ ambayo itanipa mzigo maishani mwangu” baada ya kusikia hivyo nilijiuliza ni nini maana ya kile akisemacho, “certificate ni kitu kizito mpaka kiwe mzigo namna hiyo?”  sikukawia,nilimfuata na kumuuliza  “vipi uzito wa ‘certificate uko wapi ndugu yangu maana nimesikia ukisema hutaki upate ‘certificate’ ambayo itakupa mzigo maishani mwako.’’ Alinicheka sana ,nami pia nilijiona mtu wa ajabu muno. Kwa kuwa nia yangu ilikuwa ni kutaka kujua,sikukata tamaa nilimuomba anieleze ni nini alimaanisha.Aliniambia “sitaki nipate kazi ambayo haitaleta furaha maishani mwangu,haijalishi kazi hiyo ni ndogo au kubwa.Natamani nipate kazi ambayo italeta furaha maishani mwangu,naamini nitaridhika nayo hata kama mapato yake yatakuwa ni madogo.Nafanya uchaguzi wa kazi ya kufanya kwanza ili nisije nikanung’unika kwa maisha ya baadae” Ahsanteh sana ndugu yangu nimekuelewa wanena vyema,sikujua ndugu yangu nimelipata funzo ahsanteh sana. “Bado naendelea kukuuliza hivi kwa nini ulimfanyia hivyo? Kipindi chote hicho haukutambua kuwa maisha yake umeyashikilia mikoni mwako?umeridhika kuona anataabika na amepoteza mwelekeo na dira kabisa ya maisha yake!”
Msomaji,siku moja nilikaa na kuwaza hivi kwa nini baadhi ya watu hujikana wenyewe na kuamua kufanya vitu au mambo ambayo hayana mchango wowote kwa maisha ya baadae.Wengine hupelekea kukata tamaa na kuamua kila wapatapo vijisenti huishia ‘lodge’,pombe ubadilika kuwa kinywaji cha kutulizia kiu,namaanisha ulevi wa kupindukia,maisha yao huwa hayana tumaini tena katika mioyo yao.Nilipoanza kufatilia na kufanya uchunguzi nilitambua ya kuwa kweli “unyoya haumdondoki ndege pasina sababu”.Visa ambavyo napenda nikuletee vimeambatana na swali ambalo naamini mpaka kufikia ukurasa huu wa kijitabu hiki  umekumbana nalo mara kwa mara “Bado naendelea kukuliza hivi kwa nini ulimfanyia hivyo? Kipindi chote hicho haukutambua kuwa maisha yake umeyashikilia mikononi mwako?umeridhika kuona anataabika na amepoteza mwelekeo na dira kabisa ya maisha yake!!” sipendi nikuchoshe sana kwa maandishi mengi pindi nikuleteapo visa hivi  kwani naamini “utamu wa kitabu si maandishi la! Kilichomo ndani yake” twende  sambamba ,tiririka nami mwanzo mpaka mwisho,usiachwe hata nukta pindi usomapo visa hivi.
            Mlio wa filimbi ukilia,lazima ujiulize kunani?.sauti ya Bigola ikisikika,jemedari huwasiri haraka sehemu husika.Basi nami huu ndio muda wa kukufungulia visa ambavyo vimetikisa katika kichwa changu.Kwa kuwa “tafakari ni zaidi ya takabari”,nikualike katika ukurasa wa visa hivi ,tuwe pamoja ,tutafakari pamoja kwani radha ya utunzi huu wa kijitabu hiki iko mikononi mwako msomaji.

“KWA NINI ULIMFANYIA HINYO?KIPINDI CHOTE HICHO HAUKUTAMBUA KUWA MAISHA YAKE UMEYASHIKILIA MIKONONI MWAKO?UMERIDHIKA KUONA ANATAABIKA NA AMEPOTEZA MWELEKEO NA DIRA KABISA YA MAISHA YAKE!!”
Kisa cha kwanza;FATILIA MWENDELEZO

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii